UKIONA UPO KATIKA HAYA, TAFUTA MSAADA WA HARAKA

 

1.   Haujui utambulisho wako, wewe ni nani, unaweza kufanya nini hasa, umekuja kufanya nini duniani, upi ni ubora wako, unaelekea wapi (upi ni mwisho wako). Unaharibu kesho yako kubwa, hautakuwa na manufaa yoyote katika jamii yako. Jamii yako haitajivunia kuwa na wewe, unaongeza namba ya walio hai tu.

 

2.    Unakutana kimwili na wanawake au wanaume hovyo hovyo (kabla nan je ya ndoa). Hauogopi kumpa kila mtu thamani yako. Kuna hatari hapa ya kusomba malaana, kuharibiwa hatima ya maisha, kumkosa Mungu.


3.    Unaingia mahusiano hovyo hovyo, wakati mahusiano ni maalumu kwa ajili ya kujiandaa na ndoa, unaingia tu kwa sababu wengine wameingia, ili kujifurahisha tu au kufanya zinaa. Unapoteza muda wako mwingi, unapoteza fedha, unavaa tabia zisizokusaidia maishani, unaharibi kila kitu kuhusu wewe.

 

4.    Unaishi kiholela, hauna mipango inayoeleweka ya maisha yako na haujaanza kuiishi. Hautakuwa chochote, hautafanya chochote kwenye jamii yako, na hautakuwa na kumbukumbu lolote isipokuwa kuongeza wingi wa matatizo kwenye jamii yako.

 

5.    Unampa nafasi kila mtu kwenye maisha yako, hauna uwezo wa maamuzi wa kufuatana na nani na nani siyo wa kufuatana naye. Hautajiboresha kuwa wa maana, utaishia kujua watu wengi na wote hawana faida kwako wala kwao, utaishia kujaza namba kwenye simu zisizo na matumizi, wakiwa na dakika zisizo na kazi, watakuja kumalizia kwako ili salio lao lisiende bure.

 

6.    Unakipa kila kitu nafasi, muvi zote zako, picha na video za ngono zako, kila nyimbo ya kwako, unatumia muda mwingi mtandaoni, kila kinachosemwa unataka kujua na kila post ni yako,ukiingia mtandaoni haujui umefuata ninini, popote kambi, unalala sana, unafanya vitu visivyoongeza thamani kwenye maisha yako, unataka kufanya kila kitu. Maisha yako yapo hatarini, muda wako unaliwa, unajiandaa kuwa na majuto maishani, unajiandaa kutofanya chochote, kuwa mtu wa hovyo, kuwa na tabia zisizo kusaidia popote maishani, hautakuwa na nidhamu ya maisha.

 

7.    Hauna mahusiano imara na Mungu, unahangaika na dhambi, hautaki kumpa Yesu maisha yako akusaidie, umekubali kuwa mwanadamu wa kawaida kama wengine, unaona hauwezi kuishinda dhambi kwa sababu wewe ni mwanadamu. Unaharibu nafasi ya kusaidiwa na Mungu kwenye maisha yako. Unaharibu nafasi yako kwa Mungu baada ya maisha haya. Kumbuka wewe bila Yesu si chochote popote kwa yeyote hata kama unaonekana ni wa maana, ipo siku utagundua hauna maana kwa sababu umemkosa Yesu. Hata ukijitahidi kuwa mwema kiasi gani, kama Yesu hajapata nafasi kwenye maisha yako, hakuna wemaa kwako, kuna siku hiyo dhambi uifanyayo kwa siri itafunuka, na kuharibu wema wote uliokuwa nao. Tengeneza na Mungu.

 

Comments